Salama Na podcast

Ep. 52 - Salama Na HAJI | ALIYE KUTWIKA NDIYE ATAKAYEKUTUA

2/4/2021
0:00
1:23:44
Rewind 15 seconds
Fast Forward 15 seconds

Haji Sunday Manara nlitaka kusema ni rafiki YANGU ila vacati navaza hilo nikakumbuka mmh, Haji Sunday Manara ni rafiki wa WATU WENGI hususan mashabiki wa klabu wangu pendwa na zaidi kwa watu ambao hawapendi hata mpira ila wanampenda tu jinsi anavyoseti mambo yake na anavyoigeuza sehemu yoyote aendayo kama sehemu yake ya kujitamba na kujitutumua na tofauti yake na WACHACHE ambao wanafanya kazi kama yake ni kwamba yeye anaweza KUYATEMBEA yale anayo YAONGEA.

Mapenzi yangu kwake ni ya first class na namini hata yeye analifahamu hilo, huwa namtazama kwa kuvutiwa hasa kwababu ya anavyojibeba na kukiaminisha kile ambacho anakisema, iwe kuhusu Simba, bidhaa ambayo anaitangaza au hata simulizi za maisha , vyovyote vile vitakufanya utake kumskiliza kwa umakini, na pia ni lazima ucheke. Utashi wake kwenye mambo mengi pia ni jambo la kupendeza, ukiniuliza mimi nitakuambia sawa, hata kama ni mtoto wa Kariakoo, ni watoto wa Kariakoo wangapi ambao wewe unawajua wana kipaji cha kuongea na kumfanya mtu ajiskie kama ambavyo Haji anafanya baadhi ya watu wajiskie? Iwe kwa kuzodoa au kusifia wangapi? Maneno ya papo kwa papo au hata ya kujindaa (hapo ndo utachoka kabisa), yupi?

Urafiki wetu ulianzia pale kwenye USIMBA DAMU na tuli click tu moja kwa moja, niliamini timu wangu ido kwenye mikono salama kabisa kama jina langu, tufungwe atasema maneno ya kutufanya tunyoshe mgongo na kusimama vuzuri na tukishinda well tukishinda mziki unaufahamu vizuri tu, na tukisajili je? Ahaha… Huyu mtu huya ananipa raha sana, Nba hiyo neo ilikua sababu ya Mimi na wenzangu kumvuta kitini.

Maneno mengi yamekua yakisemwa juu yake na pia mdomo wake huo ulishawahi kumtia matatani kipindi flani kile ambacho Bwana Mo Dewji alipopata matataizo, si unakumbuka? Haji alitiwa ndani siku kadhaa mpaka alipokuja kuwa cleared kwamba hakua anahusika, sikuongea nae kuhusu hilo kwasababu tu za kutotaka asiwe comfy kwenye kiti chetu ( ingawa najua ningeuliza asingekua na hiyana hata). Maneno mengine ni kuhusu urafiki wake na matajiri wa mjini ambao wengine ni wamiliki wa time pinzani za muajiri wake, hili likoje? Huwa anasumbuka wananchi wanapolileta kwenye comments za ukurasa wake maarufu wa Intagram?

Mzaliwa wa Udachini kule nchini Holland, Haji amekua hapa Dar es Salaam kwa malezi ya Bibi na Babu zake maana kipindi hicho Mzee wake alikua anakipiga nje zaidi, mimi nilitaka kujua hiyo historia yake na mpira na Mzee wake, Yanga (ambayo tunaweza kusema ni team ya familia), elimu yake na mambo ya ndoa na scandal za mitandaoni za hapa na pale. Pia tuliongelea pale alipokua wakati shabiki wa Simba Bwana Hamisi Kingwangalla alipohoji uwekezaji wa Mo Dewji na bilioni 20 za uwekezaji, na mano yake hasa kuhusu hiyo situation.

Nimecheka sana, nimeskiliza sana, nime admire sana na zaidi nimejifunza mengi ambayo nilikua siyafahamu kuhusu mtu huyo maalum na tunu ya Taifa hili. Yangu matumani utaelewa na kujifunza jambo hapa.
Tafadhaki enjoy rafiki.

Love,
Salama.

--- Support this podcast: https://podcasters.spotify.com/pod/show/yahstonetown/support

More episodes from "Salama Na"